- 20 Mei 2013
IMF yatoa wito kwa Tanzania
SHIRIKA la Fedha Duniani (IMF) limeishauri Tanzania kuongeza jitihada katika usimamizi mzuri wa sera, utakaosaidia kukuza uchumi wake na kupunguza tatizo la umasikini wa kipato, linalokabili wananchi wengi.
- 20 Mei 2013
Hakuna ushirikiano wa halmashauri, wajasiriamali
HALMASHAURI nyingi nchini zimekuwa hazitoi ushirikiano wa kutosha katika kuvitambua vikundi vya ujasiriamali wadogo, kwa kuwapatia hati za utambulisho zitakazosaidia kufungua akaunti za benki na kupata mikopo.
- 20 Mei 2013
TNBC yahitimisha majadiliano kwa wote
BAADA ya kufungwa rasmi kwa Majadiliano ya Ushirikiano kwa Wote katika ngazi ya kanda kwa mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar, Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) limesema mafanikio makubwa yamejitokeza katika ushiriki wa watu katika kutoa mawazo yao.
- 20 Mei 2013
Wakulima wa Chubi waagizwa kushirikiana na mwekezaji
WAKULIMA katika Kijiji cha Chubi Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma wametakiwa kushirikiana na mwekezaji, anayeendesha shughuli za kilimo ili waweze kujifunza ujuzi na maarifa, anayotumia kwa nia ya kuongeza uzalishaji katika mashamba yao.
- 17 Mei 2013
Biashara ya kuuza chenji hairuhusiwi
BIASHARA ya kuuza chenji hairuhusiwi kisheria, kwa kuwa shughuli hiyo inapaswa kufanywa na benki pekee. Ufafanuzi huo umetolewa leo bungeni mjini Dodoma baada ya Mbunge wa Mji Mkongwe, Muhammad Ibrahim Sanya (CUF) kutaka Serikali kudhibiti biashara ya uuzaji wa chenji inayoendelea nchini.
- 17 Mei 2013
Noah ruksa kubeba abiria
BAADA ya kilio cha muda mrefu cha baadhi ya wasafirishaji, Serikali imeruhusu magari aina ya Noah kubeba abiria nchini. Serikali imeiagiza Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), kutoa leseni hizo kwa masharti, kwa sababu magari hayo hayakuwa yameundwa kubeba abiria.


