- Created on 18 Juni 2013
Pole kwa mbunge
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema akimpa pole Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari katika Hospitali ya Selian, Arusha jana. (Picha na Veronica Mheta).
- Created on 18 Juni 2013
Ajali korongoni
Lori la mizigo lililokuwa limebeba malighafi ya kutengenezea lami, likiwa limetumbukia katika korongo eneo la Kurasini BP jijini Dar es Salaam jana baada ya dereva kushindwa kulimudu. (Picha na Mroki Mroki).
- Created on 18 Juni 2013
Kufunga tamasha
Wasanii wa kikundi cha sanaa na michezo ya asili cha Luperwa Zanzibar Group, chenye maskani yake Bububu, wakitoa burudani wakati wa hafla ya kufunga Tamasha la Mangapwani lililofungwa na Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal, Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja juzi. (Picha na Makamu wa Rais).
- Created on 17 Juni 2013
Kazi ni kazi
Waendesha baiskeli ya magurudumu matatu aina ya guta wakisukuma baiskeli zao zilizosheheni mizigo eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam jana. (Picha na Mroki Mroki).
- Created on 17 Juni 2013
Biashara bila mpangilio
Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakiendelea na biashara ya kuuza vitu mbalimbali kwa kutumia matoroli kando ya barabara ya Uhuru eneo la mzunguko wa Shule ya Uhuru jana.

