- 19 Juni 2013
Mbunge atupiana maneno na Mwenyekiti wa Bunge
MBUNGE wa Kasulu, Moses Machali (NCCR Mageuzi) jana alijikuta akitupiana maneno na Mwenyekiti wa Bunge, Jenista Mhagama bada ya kumtaka Naibu Waziri wa Fedha, Janet Mbene awe na nidhamu, kutokana na kitendo chake cha kutoa ishara ya kumdharau kwa mkono.
- 19 Juni 2013
Ajali ya basi yaua 6, yajeruhi wengi
WATU sita wanadaiwa kufa na wengine wengi kujeruhiwa kwa kukatika viungo vya mwili katika ajali ya basi, iliyotokea katika Kijiji cha Kizilamuyaga, Kata ya Kimwani wilayani Muleba mkoani Kagera.
- 19 Juni 2013
TCRA yakutana na Star TV, Star Media
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekutana na Uongozi wa Televisheni ya Star na Kampuni ya Star Media kabla ya kutoa uamuzi wake juu ya hatua ya televisheni hiyo, kujiondoa kwenye kisimbuzi cha kampuni hiyo.
- 19 Juni 2013
Serikali kudhibiti uingizwaji wa gesi
SERIKALI imesema itaendelea kuweka nguvu katika kudhibiti uingizwaji wa gesi, zinazoharibu tabaka la Ozoni.
- 19 Juni 2013
Mahakama ya Rufaa yaita jalada kesi ya Lwakatare, mwenzake
MAHAKAMA ya Rufaa Dar es Salaam imeita majalada ya kesi ya Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema Wilfred Lwakatare na mwenzake Ludovick Joseph kwa ajili ya kufanya marejeo ya uamuzi wa Mahakama Kuu uliowafutia washitakiwa hao mashitaka ya ugaidi.
- 19 Juni 2013
Mbunge ataka Serikali kuwakamua kodi zaidi wananchi
WAKATI wabunge mbalimbali pamoja na Kamati ya Bunge ya Bajeti, wakipendekeza baadhi ya kodi kuondolewa, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ally Keissy Mohamed (CCM) ameitaka Serikali iwakamue vilivyo wananchi.


