Arsenal yampandia dau Havertz

ARSENAL imeongeza dau hadi kufikia pauni milioni 60 wakitaka huduma ya kiungo Kai Havertz kutoka Chelsea.

Mjerumani huyo ameonesha nia ya kusepa Chelsea hata hivyo bado klabu yake haijathibitisha kukubaliana na dau hilo.

Havertz alijiunga na Chelsea 2020 kwa dau la pauni milioni 85 na kusaini mkataba wa miaka mitano.

Advertisement

Mpaka sasa mkataba wa nyota huyo umebaki miaka miwili hata hivyo hana nia ya kuendelea kucheza klabuni hapo.

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *