Abood aongeza nguvu kusaidia jamii sekta ya elimu, afya

MBUNGE wa Jimbo la Morogoro Mjini, Abdulaziz Abood ameahidi kutengeneza madawati 400 kwa lengo la  kupunguza uhaba unaozikabili  shule za  kata ya  Mwembesongo na Kingolwira.

Abood ametoa ahadi hiyo  kwenye  ziara yake ya  kusikiliza changamoto za wananchi katika  kata hizo  ikiwa na  utekelezaji wa Ilani Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kulikiliza na kutatua kero cha wananchi.

Licha ya kutoa  ahadi hiyo, akiwa kata ya Kingolwira alikabidhi shuka 30 kwa ajili ya matumizi ya wagonjwa wa  Kituo cha Afya  Kingolwira baada ya kupata taarifa ya uwepo wa upungufu mkubwa wa shuka.

Advertisement

Mbunge huyo alikabidhi shuka hizo kwa Diwani wa kata hiyo ,Madaraka Bidyanguze pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Kituo cha Afya, Simba Waziri wakiwemo na viongozi wengine wa CCM.

Abood  aliahidi kukarabati madirisha  ya zamani 15 yenye nyavu na kuweka  mapya  ya vioo vya aluminium katika   wodi ya wanawake na  ya wanaume , ununuzi wa mashine ya kufuria shuka  na mabenchi saba ya kukalia wagonjwa kwenye kituo hicho.

Kwa upande wa Vikundi vya Ujasiliamali, Mbunge huyo alikabidhi hundi ya milioni moja (sh 1000,000 ) kwa ajili ya kukuza mtaji wa wanawake  Wajasiliamali  wa Kikundi cha Umoja ni Ushindi wanaofanya biashara soko la Kingolwira .

“  Nimefika hapa pamoja na mambo mengine lakini niliwaahidi  kuwapatia fedha za kuimalisha  mtaji wa kikundi chenu   na leo ninawakaabidhi hundi  y a sh milioni moja ya kuendeleza biashara zetu hapa sokoni Kingolwira” alisema Abood

Kwa upande wao wanawake wa kikundi hicho kpitia kwa mwenyekiti wake , Fatuma Omary alimshukuru mbunge Abood kwa kuwawezesha fedha kwa ajili ya kuboresha mtaji wao ili kukundi chao kuweze kuwa na maendeleo makubwa .

“ Tunamshukuru mheshimiwa mbunge wetu kwa kutupatia mtaji wa Sh milioni moja , sisi wanachama wakikundi hiki ambao ni wanawake 40 , tutatumia mtaji huu kuuendeleza zaidi tuweze kuinuka kiuchumi na kuwasaidia watoto wetu “ alisema Fatuma.

Katika hatua nyingine Mbunge Abood aliwapatia samani za Ofisi ya Wanawake wa CCM Kata ya Kingolwira Meza, Viti na Vitu vingine vya kiofisi ili iweze kuwa hadhi zaidi.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *