Al-Ahly watua kibabe

KLABU ya Al-Ahly ya Misri imefika nchini usiku wa leo ikiwa ni maandalizi kuelekea mchezo wa African Football League dhidi ya Simba SC.

Mabingwa hao mara 11 wa Ligi ya Mabingwa Afrika, watacheza mchezo huo wa ufunguzi kesho Ijumaa katika uwanja wa Mkapa.

Ikumbukwe, timu hiyo itakutana na timu mbili kubwa za Tanzania kwenye michuano miwili mikubwa tofauti.

Itakutana na Yanga pia kwenye mchezo wa kundi D, linalojumuisha timu za Al-Ahly, Belouzdad na Medeama ya Ghana.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *