Asas ajiunga rasmi Red Cross

Asas ajiunga rasmi Readcross

MFANYABIASHARA  na mmiliki wa kampuni za ASAS Group, Salim Abri (ASAS) amejiunga rasmi na uanachama wa maisha  wa Shirika la Msalaba Mwekundu Tanzania ‘Red Cross’.

Rais wa Redcross ambaye pia ni Mbunge wa Mufundi, Kusini David Kihenzile, ameiambia HabariLeo kuwa Asas mbali na kujiunga rasmi kuwa mwanachama wa Red Cross, pia amechangia fedha taslimu Sh milioni 5 kwa ajili ya kambi ya vijana wa shirika hilo.

Advertisement

 

Kihenzile amesema Tanzania Red Cross Society inafanya kazi kwa bidii na kutoa huduma za kibinadamu   kwa kufuata kanuni  zake saba za  ubinadamu, uadilifu,  kutopendelea, uhuru, kujitolea, umoja, na kushirikiana kimataifa, hii inaifanya jamii kuiamini na kulisaidia shirika  kutimiza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.

Kwa upande wa Asas, amepongeza Baraza la Vijana na uongozi wote wa Redcross chini ya Rais wake David Kihenzile na kudai kuwa ni kiongozi mwenye maono anatoa matokeo na ameipaisha  Redcross kitaifa na kimataifa

Pia amewaahidi vijana kushirikiana nao katika kujenga moyo wa kujitolea kwa Watanzania, kazi ambayo Red Cross wanaifanya.

 

 

 

 

 

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *