Baba Ramsdale: Carragher kuwa na heshima

KAULI za kibaguzi za baadhi ya wadau wa soka duniani kwa wachezaji zinaendelea kuchukuwa sura mpya kwa wazazi wa wachezaji.
Wiki mbili zilizopita, Zoe Maguire, mama wa beki Harry Maguire alichukizwa na kauli za kibaguzi dhidi ya mtoto wake kufuatia kiwango kisichoridhisha cha mchezaji huyo wa Manchester United.
Katika muendelezo wa wazazi kuchukizwa na kauli hizo, Nick Ramsdale, baba mzazi wa kipa wa Arsenal, Aaron Ramsdale amechukizwa na kauli ya beki wa zamani wa Liverpool, Jamie Carragher ambaye kwa sasa ni mchambuzi wa michezo Skysport.
Katika mchezo wa EPL, Arsenal dhidi ya Spurs uliopigwa Jana Emirates, kocha wa Arsenal, Mikel Arteta aliendelea kumpa nafasi kipa mpya David Raya na kumuacha benchi Aaron Ramsdale, wakati mpira ukiendelea kipindi cha kwanza, Ramsdale alimpigia makofi Raya baada ya kuokoa mpira ambao wengi hawakutegemea.
Kitendo cha kupiga makofi kilimfanya Carragher kutoa kauli: “Unajua mtu anapopoteza Oscar na kuanza kupiga makofi na kutabasamu kwa ajili ya mtu mwingine.” Kauli hiyo imetafsiriwa kuwa ya kibaguzi na kupelekea baba wa mchezaji huyo kutoa kauli.
“Wewe umekosa heshima onyesha daraja fulani vijana wangu.” Aliandika Nick.
Katika mchezo huo Arsenal ilipata sare ya pili msimu huu ya mabao 2-2 na hivyo kuwa na pointi 14.
Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet…
Check The Details HERE….. https://smartcareer12.blogspot.com/
I’m making $90 an hour working from home. I never imagined that it was honest to goodness yet my closest companion is earning 16,000 US dollars a month by working on the connection, that was truly astounding for me, she prescribed for me to attempt it simply. Everybody must try this job now by just using this website… http://Www.Smartwork1.Com