Bakwata: Tuna imani kubwa na serikali

DODOMA: BARAZA Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata) limesema linamuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan na serikali yote na kuwaombea dua ili waweze kuwa na ufanisi zaidi.
Akisoma salamu za Bakwata katika Baraza la Maulid Kitaifa mkoani Dodoma leo Septemba 28, 2023, Katibu Mkuu wa Bakwata Alhaj Nuhu Mruma amesema, sababu za wao kuiunga mkono serikali ni kutokana na juhudi inazofanya katika kuwaletea maendeleo wananchi.
“Serikali imekuwa ikiwaletea wananchi maendeleo kwenye sekta za kiuchumi, kisiasa na kijamii pamoja na kuboresha mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini, hatuna budi kuiunga mkono,”amesema.
Amesema katika kujenga demokrasia nchini, Rais Samia Suluhu Hassan aliunda kikosi kazi maalum kilichoshughulikia masuala ya demokrasia na hatimaye kuyakubali maoni mengi yaliyopendekezwa na kikosi kazi hicho.
“Na mengine yameanza kufanyiwa kazi ikiwemo ruhusa ya vyama vya siasa kufanya mikutano yao ya hadhara, tunampongeza sana Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan,” amesema Mruma.
Amesema jukumu lao viongozi wa dini ni kuendelea kuishauri serikali, kushirikiana na serikali katika utekelezaji wa mambo mbalimbali na kuiombea amani nchi pamoja na kuwaombea viongozi wake.
I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com
The first check I got was for $13,000. I feel so inspired even though I haven’t really made much progress up till now. I’m looking forward to the episode of the next week with anticipation now that I know I need to work harder.
.
.
Detail Here————————————————————>>> http://Www.BizWork1.Com