Barabara ya Mlima Kitonga kupanuliwa

HATIMAYE serikali imesikia kilio cha Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Iringa cha kufanya upanuzi wa barabara katika mlima wa Kitonga, wilayani Kilolo mkoani humo.

Kwa muda mrefu kamati hiyo inayoongozwa na Salim Asas imekuwa ikiiomba serikali ama kupanua barabara hiyo au kujenga barabara nyingine ya mchepuo ili kupunguza ajali na foleni ya magari yanayosafiri ndani na nje ya nchi.

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa leo ametembelea barabara hiyo yenye mlima mkali na akatoa taarifa ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya upanuzi huo.

Katika ziara hiyo aliyoambatana na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Usalama Barabarani, viongozi wa chama na serikali na wabunge, Bashungwa amesema serikali imetenga zaidi ya Sh bilioni 6.4 kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huo ikiwa ni suluhisho la muda mfupi la kukabiliana na changamoto hizo katika mlima huo.

“Serikali inatambua umuhimu wa barabara hii kwa maendeleo ya sektaya usafirishaji na uchumi wa nchi. Ni barabara iliyopo katika mipango yetu na tuahidi kwamba changamoto zake zitaendela kufanyiwa kazi,” alisema.

Awali Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) Mkoa wa Iringa, Mhadisi Yudas Msangi alisema kwa kutumia fedha hizo jumla ya mita 1600 za Mlima Kitonga zitatanuliwa ili kupunguza foleni na ajali katika eneo hilo la barabara hiyo ya Tanzania Zambia (TANZAM).

Mhandisi Msangi alizungumzia suluhusho la muda mrefu la barabara hiyo akisema Oktoba 3, mwaka huu Tanroads ilisaini mkataba wa usanifu wa kina wa upanuzi wa Mlima Kitonga.

“Hadidu za rejea za mradi huu zinamtaka mhandisi mshauri kuona uwezekano wa kupata njia mbadala ya kudumu inayokadiriwa kuwa ya kilometa 31 itakayopita katika vijiji vya Mlowa, Mifugo, Mlafu na Ilula ili kupunguza changamoto katika mlima huo,” alisema.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Iringa, Salim Asas aliishukuru serikali kwa kusikia kilio cha kamati yake akisema lengo lao ni kufanya barabara za mkoa wa Iringa zipitike wakati wote na kwa usalama.

Asas alizungumzia changamoto za barabara hiyo akisema barabara pana zinaweza kuwa na njia nyingi za kuingia na kutoka, na kuongeza nafasi ya kuona magari mengine hatua inayoweza kupunguza hatari ya ajali na foleni.

Pamoja na kushukuru kwa mpango huo, Asas alisema ni muhimi ikazingatiwa kuwa kupanua barabara pekee haitoshi kuzuia ajali.

“Elimu ya usalama wa barabarani, utekelezaji wa sheria za barabarani, na utunzaji wa magari ni muhimu pia katika kuboresha usalama wa barabarani,” alisema.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Halima Dendego kwa upande wake amesema kuboreshwa kwa barabara hiyo kutachochea utalii kusini mwa Tanzania.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
11 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
JaylenJordin
JaylenJordin
1 month ago

★ I’m making $90 an hour working from home. ( q66q) i was greatly surprised at the same time as my neighbour advised me she changed into averaging $100 however I see the way it works now. I experience mass freedom now that I’m my non-public boss. Everybody must try this job now by just using this website..
CLICK HERE ——————->> http://smartcareer2.blogspot.com

Last edited 1 month ago by JaylenJordin
Julia
Julia
1 month ago

Cash generating easy and fast method to work part time and earn an extra $15,000 or even more than this online. By working in my spare time I made $17990 in my previous month and I am very happy now because of this job. you can try this now by following 

the details here…… http://Www.Smartcash1.com

Last edited 1 month ago by Julia
Angelhompson
Angelhompson
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by Angelhompson
MONEY
MONEY
1 month ago

UBUNIFU – ALILIA NA KUPAMBANA KUANDIKWA/KUYAUWA MAGAZETI YA GROBAL PUBLISHER

R.jpeg
MONEY
MONEY
1 month ago

UBUNIFU – ALILIA NA KUPAMBANA KUANDIKWA/KUYAUWA MAGAZETI YA GROBAL PUBLISHER ..

11.jpg
MONEY
MONEY
1 month ago

UBUNIFU – ALILIA NA KUPAMBANA KUANDIKWA/KUYAUWA MAGAZETI YA GROBAL PUBLISHER /

Screenshot_20190909-051939.jpg
MONEY
MONEY
1 month ago

UBUNIFU – ALILIA NA KUPAMBANA KUANDIKWA/KUYAUWA MAGAZETI YA GROBAL PUBLISHER //

leo.jpg
MONEY
MONEY
1 month ago

UBUNIFU – ALILIA NA KUPAMBANA KUANDIKWA/KUYAUWA MAGAZETI YA GROBAL PUBLISHER “

Screenshot_20190809-051607.jpg
MONEY
MONEY
1 month ago

UBUNIFU – ALILIA NA KUPAMBANA KUANDIKWA/KUYAUWA MAGAZETI YA GROBAL PUBLISHER ….

Screenshot_20190809-051607.jpg
MONEY
MONEY
1 month ago

UBUNIFU – ALILIA NA KUPAMBANA KUANDIKWA/KUYAUWA MAGAZETI YA GROBAL PUBLISHER ……

OIP (2).jpeg
MONEY
MONEY
1 month ago

UBUNIFU – ALILIA NA KUPAMBANA KUANDIKWA/KUYAUWA MAGAZETI YA GROBAL PUBLISHER \”

OIP (1).jpeg
Back to top button
11
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x