Baraza UDSM kufuatilia ujenzi majengo 21

BARAZA la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) limejipanga kufuatilia utekelezaji wa mradi ujenzi wa majengo 21 ya chuo hicho chini ya Mradi wa Mageuzi ya Kiuchumi Elimu ya Juu (HEET).

Mwenyekiti wa baraza hilo, Balozi Mwanaidi Maajar amesema hayo wakati wa utiaji saini mikataba miwili ya usimamizi ujenzi wa majengo hayo yatakayojengwa kwenye maeneo mbalimbali ya Chuo Kikuu cha Dare es Salaam yaliyopo Dar es Salaam, Lindi na Zanzibar.

Amesema baraza litahakikisha utekelezaji wa mradi huo unafanyika kwa weledi na uadilifu ili kuhakikisha kuwa utekelezaji huo unakamilika kwa wakati, kulingana na muda uliowekwa .

“Tunasisitiza kuwa kila mmoja anayehusika kwa namna moja au nyingine katika utekelezaji wa mradi huu atimize wajibu wake kwa ufanisi inavyopaswa na kwa wakati unaotakiwa,” amesema.

Naye Makamu Mkuu wa UDSM, Profesa William Anangisye amesema timu ya wataalamu katika chuo hicho imefanya kazi kubwa ya kuandaa michoro, kuiwasilisha kwa wadau na watumiaji wa majengo, kuifanyia marekebisho na kisha kupitishwa na baraza.

“Ni matumaini yetu kuwa majengo haya yatakidhi mahitaji yote muhimu ya wakati huu katika miundombinu ya kufundishia na kujifunzia. Wajenzi na wasimamizi wa ujenzi wahakikishe kuwa tunapata majengo bora na ya kisasa,” amesema.

Naibu Makamu Mkuu wa UDSM upande wa Mipango, Fedha na Utawala Profesa Bernadeta Killian amesema chuo hicho kimetengewa kiasi cha Dola milioni 47.5 sawa na Sh bilioni 110 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa HEET kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia Juni 2021 hadi Julai 2026.

“Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinatekeleza mradi kupitia fani za vipaumbele vya taifa ambazo ni pamoja na uhandisi na teknolojia; TEHAMA, mipango miji, uhandisi wa mazingira na teknolojia, kilimo na kilimo biashara, utalii na ukarimu.

Kwa upande wake Naibu Mratibu wa Mradi wa HEET, Dk Liberato Haule amesema Mikataba itahusu washauri elekezi wawili ambao ni Arqes Africa Architects & Interior Designers Limited na Geometry Consultants Limited

Amesema Mshauri Elekezi Arqes Africa Architects & Interior Designers Limited atasimamia kazi 10 na mshauri Mwelekezi Geometry Consultants Limited atasimamia kazi 11 .

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
MeghanSmith
MeghanSmith
1 month ago

Everybody can earn 500 dollars daily. Yes! you can earn more than you think by working online from home. I have been doing this job for like a few weeks and my last week payment was exactly 30,000 dollars.
.
.
Detail Here———————————————————->>>  http://Www.BizWork1.Com

Angila
Angila
1 month ago

In 2023 many people are now joining online jobs very fast because it has potential. i joined this 3 months ago and in 3 months I totally received $50743 and all I was doing is copy and paste stuff in my part time. Join now and start making money:-

.
.
.
From this website: …> > > http://remarkableincome09.blogspot.com

SamanthaKeenan
SamanthaKeenan
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by SamanthaKeenan
Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x