Bashungwa awapa somo wahitimu mafunzo ya ulinzi

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Innocent Bashungwa  amewataka wahitimu 65 wa kozi ya stashahada ya kawaida ya masomo ya ulinzi na usalama sanjari na shahada ya uzamili ya sanaa katika masomo ya ulinzi na usalama,  kuwawezesha  kufikiria na kuchambua matatizo ya usalama, katika mtazamo wa kijeshi.

Bashungwa ameyasema hayo wakati wa kutunuku maofisa hao  wa kozi ya 37  ya mwaka  2022/23 kwa maofisa wanafunzi 65  kutoka Chuo Cha Ukamanda na Unadhimu (CSC)kilichopo Duluti Wilayani Arumeru, mkoani Arusha.

Amesema mafunzo hayo yamewashirikisha wahitimu Watanzania 46,  pamoja na maofisa wanafunzi 19 kutoka nchi marafiki na kuongeza kuwa   maarifa waliyopata kupitia mafunzo hayo  yatawawezesha kufikiria na kuchambua matatizo ya usalama, katika mtazamo wa kijeshi.

 

“Hayati Julius Kambarage Nyerere, muasisi wa taifa letu la Tanzania aliwahi kusema kuwa, ‘bila Umoja, hakuna mustakabali wa Afrika’,sambamba na maneno hayo ya hekima kutoka kwa Mwalimu Nyerere, Tanzania ina uhusiano mzuri sana na wa kirafiki na nchi nyingine,” amesema.

Pia amewapongeza wahitimu wanawake waliohitimu  mafunzo hayo  na kuongeza kuwa uwepo wa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Rais  ni hatua muhimu kwa  Tanzania kuelekea usawa wa kijinsia.

Amesema uongozi wake makini unatuma ujumbe mzito kuhusu uwezo wa uongozi wa wanawake, na umuhimu wa kuwapa wanawake fursa sawa kwa maendeleo ya mataifa.

Awali Mkuu wa chuo cha Ukamanda na Unadhimu(CSC) Brigedia Jenerali,Sylivester Ghuliku alisisitiza kuwa chuo hicho kitaendelea kushirikiana na nchi mbalimbali kwa ajili ya utoaji mafunzo ya kijeshi na kiutawala.

Wahitimu wengine wanatoka  nchi  za   Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),  Misri, Kenya, Eswatini, Malawi,  Msumbiji,Nigeria,  Rwanda,Afrika Kusini na Uganda.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments
Back to top button
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x