Bayern, PSG watangulia robo UEFA

BAYERN Munchen na PSG zimekuwa timu za kwanza kufuzu robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, baada ya ushindi wao wa mechi za usiku wa leo.

Bayern ilishinda bao 3-0 dhidi ya Lazio na hivyo kupindua matokeo ya 1-0 ya wiki mbili zilizopita. PSG ikiwa Reale Arena iliipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Real Sociedad na hivyo kwenda robo kwa ushindi wa mabao 4-1, baada ya ushindi wa 2-0 wiki mbili nyuma.

Mshambuliaji wa Bayern Munchen, Harry Kane alifunga mabao mawili, katika ushindi huo, Thomas Muller aliweka kambani bao moja.

Advertisement

Kwa upande wa PSG, Kylian Mbappe alifunga mabao mawili.