RAIS wa Marekani Joe Biden ametangaza mipango ya kuzuru nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara hivi karibuni ikiwa ni mkakati wa Marekani kupanua uwepo wake katika eneo hilo na kukabiliana na ushawishi wa Urusi na China.
“Sote tutakuwa tunakuona na utatuona wengi,” Biden aliwaambia viongozi wa Afrika karibu 50 alipohudhuria siku ya tatu ya mkutano wa kilele wa Marekani na Afrika katika mji mkuu wa Marekani.
Ziara hiyo itakuwa ya kwanza kwa Biden Kusini mwa Jangwa la Sahara tangu awe Rais. Ingekuwa karibu ziara yake ya kwanza rasmi katika bara hilo, ukiachia aliposimama kwa muda mwezi Novemba nchini Misri.
Biden ameangazia ziara zake za nje kwa nchi za Asia na Ulaya katika miaka miwili ambayo amekuwa Rais, huku akitaka kuimarisha uhusiano wa Indo-Pasifiki na kuratibu umoja wa magharibi dhidi ya Urusi, na kwa haraka zaidi Uchina.
Thank you for your sharing. I am worried that I lack creative ideas. It is your article that makes me full of hope. Thank you. But, I have a question, can you help me?