BUNGE la Tanzania limempongeza Naibu Waziri Mkuu, Dk.
Dotto Biteko kwa kuteuliwa kushika wadhifa huo.
Akitoa pongezi hizo bungeni mjini Dodoma leo, muda mfupi baada ya Dk Biteko kuingia ukumbini kwa mara ya kwanza tangu aapishwe kushika wadhifa huo Ijumaa iliyopita, Spika Dk Tulia amesema kwa niaba ya Bunge na Watanzania kwa ujumla wanampongeza kwa kuaminiwa na Rais kushika wadhifa huo.
Amemuahidi ushirikiano wa kutosha katika majukumu yake mapya, kama ambavyo walikuwa wakimpa siku zote.
Dk Tulia amesema nafasi hiyo ya Naibu Waziri Mkuu ni ya kihistoria, inatokea kwa wachache, ambapo yeye ni miongoni mwao, hivyo kumtakia kila la heri.
Comments are closed.