CCM yatoa mwelekeo wa vijana 2030

DAR ES SALAAM: MAKAMU Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Taifa (UVCCM) Rehema Sombi, amesema CCM imeendelea kuisimamia serikali kuchukua hatua za kujenga ustawi na maendeleo ya jamii kwa kuimarisha huduma kwa makundi maalumu likiwemo la watu wenye ulemavu, vijana, watoto, wanawake na wazee.

Rehema ameyasema hayo leo Septemba 25, 2023 katika kikao kilichoambatana na hafla ya kampeni ya uwekaji wa bendera ya malengo ya maendeleo endelevu (Sustainable Development Goals – SDGs) iliyofanyika katika jengo la Umoja House – Ubalozi wa Netherlands.


Amesema baadhi ya hatua zilizochukuliwa ni kuendelea kutoa ruzuku kwa taasisi za watu wenye ulemavu kila mwaka na kutoa vitendea kazi, pamoja na kuanzisha mfuko maalumu wa watu wenye ulemavu kwa lengo la kuwawezesha kiuchumi ikiwa ni sera za mwelekezo wa CCM 2020 -2030.

“Hatua nyingine ni kutekeleza Sera ya jinsia ya mwaka 2016 ambayo inatoa mwongozo wa kusimamia masuala yote ya wanawake nchini, kuanzisha mtandao wa wajasiriamali wanawake na kutekeleza mpango kazi wa miaka mitano wa kupambana na ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto (2017 – 2022),” amesema.

Pia, ametaja hatua nyingine ni kutoa mafunzo ya stadi za maisha kwa vijana 79,675 na kuviwezesha vikundi vya vijana 796 vinavyojishughulisha na kilimo, ufugaji na ushoni kupata mikopo kupitia mfuko wa uwezeshaji hivyo kufanikiwa kujiajiri katika maeneo ya kilimo.


Pamoja na hayo ameonyesha msimamo wa serikali katika kuweka mkazo juu ya masuala ya elimu hususani ya sayansi kwa wasichana.

Aidha, amesema serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeweka juhudi kubwa kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu hususan kupitia ujenzi wa miundombinu wezeshi ya kimaendeleo na kushirikisha vijana katika ukuzaji uchumi kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Mkutano huo umeongozwa na Balozi wa Netherlands nchini Tanzania Wiebe De Boer ambaye amesisitiza kuwa vijana ndilo kundi muhimu kwa mabadiliko ya maendeleo kwa nchi yao.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
JenniferWilliam
JenniferWilliam
2 months ago

Earn income while simply working online. work from home whenever you want. just for maximum 5 hours a day you can make more than $600 per day online. From this I made $18,000 last month in my spare time.
.
.
Detail Here———————————————————————————->>>  http://Www.BizWork1.Com

Lalaerin
Lalaerin
2 months ago

I even have made $17,180 only in 30 days straightforwardly working a few easy tasks through my PC. Just when I have lost my office position, I was so perturbed but at last I’ve found this simple on-line employment & this way I could collect thousands simply from home. Any individual can try this best job and get more money online going this article…..
>>>>>   http://Www.Careers12.com

Last edited 2 months ago by Lalaerin
money
money
2 months ago

Mashindano ya nani kuhinda kwenye neno “ABROAD“ NCHINI TANZANIA!?

MJERUMANI

MHINDI

MTANZANIA

MKENYA

MNIGERIA

MHISPANIA

file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg

NANI AINGIZE NDEGE ZA KWENDA KUMSALIMIA BABU NA BIBI, KWA ALIYESHINDA KULELEWA NA BIBI TU!?

Capture.JPG
Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x