Chongolo ataka majina wasiolipwa fidia

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kondoa kumpa orodha ya wananchi ambao wamevamiwa na wanyama wakali na waharibifu na mpaka sasa hawajalipwa fidia.
Akiwa katika siku yake ya tano ya ziara katika majimbo ya Mkoa wa Dodoma, Chongolo ametaka orodha hiyo aipate kabla ya kumaliza ziara yake mkoani Dodoma.
Kauli ya Chongolo ameitoa kutokana na wananchi kubainisha uwepo wa changamoto ya uharibifu wa mazao yao kutokana na tembo na kutaka nguvu inayotumika kuwalipisha fidia wananchi pindi wanapokuwa wameingiza mifugo hifadhini, ndio itumike kulipa fidia wanapoathiriwa na tembo.
“Nataka nipewe orodha ya watu wote ambao wameathiriwa na wanyama wakali na wahalibifu kabla sijamalizia ziara yangu, halafu nimjue huyo anayekwamisha watu kulipwa fidia.”
Chongolo aliwashangaa watendaji ambao wanashindwa kuwajibika kufanya tathimin ya uharibifu unapotokea na kuwa kitendo hicho ni kuwachonganisha wananchi na serikali yao na kuchonganisha wananchi na CCM.
Chongolo aliwataka watendaji kuhakikisha wanafanya tathimini halisi na kwa wakati, ili wananchi waweze kufidiwa kutokana na madhara waliyoyapata.
[๐๐จ๐ฐ ๐๐จ ๐๐๐ค๐ ๐๐ฑ๐ญ๐ซ๐ ๐๐ง๐๐จ๐ฆ๐ ๐ ๐ซ๐จ๐ฆ ๐๐จ๐ฆ๐ ๐๐ก๐๐ง๐ ๐ ๐๐จ๐ฎ๐ซ ๐๐ข๐๐ ๐๐๐]ๅฝกโ
๐๐จ๐จ๐ ๐ฅ๐ ๐ข๐ฌ ๐ฉ๐ซ๐๐ฌ๐๐ง๐ญ๐ฅ๐ฒ ๐ฉ๐๐ฒ๐ข๐ง๐ $๐๐,๐๐๐ ๐ญ๐จ $๐๐,๐๐๐ ๐๐ฏ๐๐ซ๐ฒ ๐ฆ๐จ๐ง๐ญ๐ก ๐๐จ๐ซ ๐ฐ๐จ๐ซ๐ค๐ข๐ง๐ ๐จ๐ง ๐ญ๐ก๐ ๐ฐ๐๐ ๐๐ซ๐จ๐ฆ ๐ก๐จ๐ฆ๐. ๐ ๐ก๐๐ฏ๐ ๐ฃ๐จ๐ข๐ง๐๐ ๐ญ๐ก๐ข๐ฌ ๐๐๐ญ๐ข๐ฏ๐ข๐ญ๐ฒ ๐ ๐ฆ๐จ๐ง๐ญ๐ก๐ฌ ๐๐๐๐ค ๐๐ง๐ ๐ ๐ก๐๐ฏ๐ ๐๐๐ซ๐ง๐๐ $๐๐,๐๐๐ ๐ข๐ง ๐ฆ๐ฒ ๐๐ข๐ซ๐ฌ๐ญ ๐ฆ๐จ๐ง๐ญ๐ก ๐๐ซ๐จ๐ฆ ๐ญ๐ก๐ข๐ฌ ๐๐๐ญ๐ข๐ฏ๐ข๐ญ๐ฒ. ๐ ๐๐๐ง ๐ฌ๐๐ฒ ๐ฆ๐ฒ ๐ฅ๐ข๐๐ ๐ข๐ฌ ๐ข๐ฆ๐ฉ๐ซ๐จ๐ฏ๐๐ ๐ญ๐จ๐ญ๐๐ฅ๐ฅ๐ฒ!
.
.
๐๐จ๐จ๐ค ๐๐ญ ๐ข๐ญ ๐ฐ๐ก๐๐ญ ๐ ๐๐จ—————————->> http://www.join.hiring9.com