Chuo Kikuu Mzumbe wazindua dawati la jinsia

Chuo Kikuu Mzumbe wazindua dawati la jinsia

CHUO Kikuu Mzumbe  kilichopo mkoani Morogoro, kimezindua ofisi maalumu ya dawati ya jinsia, ili  kutimiza malengo ya serikali ya kupunguza na kumaliza kabisa  vitendo vya ukatili wa kijinsia  katika vyuo vikuu na  kwenye jamii nchini.

Hatua ya uzinduzi wa ofisi ya dawati hilo ni utekelezaji wa agizo la serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wanawake na Makundi Maalum kwa lengo la madawati hayo kuwa na majukumu ya kutokomeza aina zote za ukatili maeneo ya vyuo.

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu hicho, Profesa  William Mwegoha,  amesema  hayo  Machi 23,2023 chuoni hapo kwenye  hotuba yake kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Fatma Mwassa  kwenye uzinduzi dawati hilo  kampasi kuu ya Morogoro. Mkuu wa Mkoa aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Rebeca Nsemwa.

Advertisement

Profesa Mwegoha amesema  uongozi wa chuo hicho umetoa jengo ,  kulikarabati  na ununuzi wa vifaa  kwa ajili ya matumizi ya wajumbe walioteuliwa wa dawati hilo, ambalo litafanya kazi kwa kuzingatia mwongozo  wa serikali.

 

Ametaja njia zitakazotumika kupata taarifa za unyanyasaji wa kijinsia ni pamoja na mlengwa kufika moja kwa moja kwenye ofisi za dawati la jinsia, kupiga simu kupitia namba ya wazi ambayo mtu yeyote anaweza kupiga na kutoa taarifa zake kwa njia ya barua pepe na kutumia sanduku la maoni.

Naye  Mkuu wa Wilaya ya Morogoro , Nsemwa  kwa niaba ya mkuu wa mkoa amesema, hivi sasa kumekuwa na ongezeko kubwa la matukio yanayohusiana na unyanyasaji wa kinsia na mashambulio ya aibu yanayohusisha wana familia na jamii kwa ujumla.

Amesema  dawati hilo la jinsia  liwe chachu kutokomeza ukatili wa  jinsia chuoni, huku akiwataka wajumbe wa dawati hilo  kutunza siri na kutoa msaada unaostahili kwa waathiriwa wa unyanyasaji wa kijinsia, ili kujenga jamii iliyo bora.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *