DC Karagwe atoa maagizo mradi wa maji Kibwela

DC Karagwe atoa maagizo mradi wa maji Kibwela

MKUU wa Wilaya ya Karagwe,  Julius Laiser ameagiza kuondoka wananchi wanaofanya shughuli za kibinadam katika chanzo  cha maji mradi wa Kibwela.

Akiweka jiwe la msingi katika mradi wa maji wa Kibwela, ambao umevamiwa na wanachi  wanaoendesha shughuli za kilimo, Mkuu huyo wa wilaya, alisema serikali imekuwa ikiwekeza fedha nyingi  katika miradi ya maji kwa ajili ya wananchi, lakini wananchi wenyewe ndio chanzo kikubwa cha kuharibu miundombinu na kusababisha maji kukauka.

Advertisement

” Moja ya changamoto kubwa katika miaka iliyopita ni upatikanaji wa maji safi na salama , serikali iliunda chombo cha kusimamia miradi ya maji vijijini (RUWASA),  lakini niseme tu sisi wenyewe tunaharibu.

“Mimi kama mwakilishi wa serikali sitakubali hujuma au uharibifu wa kazi iliyosimamiwa vizuri, lazima wananchi waheshimu sheria na wachukulie miradi hii kama miradi yao na vizazi vijavyo,”alisema Laizer.

Ametoa wito kwa mamlaka zinazosimamia miradi ya maji wilayani  Karagwe kuhakikisha miradi ya maji inapokamilika panakuwepo na maeneo ya kunyweshea mifugo, ili  kuhakikisha wafugaji hawatumii maeneo ya vyanzo vya maji kunyweshea mifugo yao.

Kaimu Meneja wa RUWASA, Justo Mutabuzi  amesema mradi huo  umepunguza changamoto  ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi na kuifanya Wilaya ya Karagwe kufikia asilimia 74 ya upatinaji  wa maji safi na salama.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *