NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Doto Biteko amekabidhi Bima za Afya za bure kwa Wananchi 6,000 wa jiji la Mbeya.
Bima hizo zimetolewa na Taasisi ya Tulia Trust kupitia Mkurugenzi wa taasisi hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini, Dk Tulia Ackson.
Hatua hiyo ni muendelezo wa msaada ambao Dk Tulia amekuwa akiutoa kila mwaka kwa Wananchi wake.