MKOA wa Dodoma umempongeza Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuondoa katazo la mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa.
Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, Alhaji Adam Kimbisa na kuongeza kuwa fursa hiyo itasaidia kueleza mafanikio mengi ambayo serikali ya Awamu ya Sita inayetekeleza ikiwemo ujenzi wa madarasa, hospitali, barabara na hata madaraja.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Januari 5, 2023. Mwenyekiti huyo amesema uamuzi huo ni hatua kubwa katika kupata maendeleo.