DPO Pay yapata leseni Tanzania

KAMPUNI ya DPO Pay inayotoa huduma za malipo ya kidijitali imetambuliwa na kupewa kibali na Benki Kuu ya Tanzania kuendesha huduma zake.

DPO Pay yenye makao makuu yake nchini Kenya, itaendeleza shughuli zake nchini baada ya kuwa imetambuliwa kwa mujibu wa sheria na kupata leseni.

Tumefurahi kupokea leseni hii kutoka kwa Benki Kuu ya Tanzania. Kwa kuzingatia dhamira yetu thabiti yakuongeza wigo wa utoaji huduma zetu katika nchi za Afrika Mashariki, kibali hiki ni sehemu yakuonesha nia yetu na uthabiti wetu wa kufuata taratibu zote za kisheria na kiutaratibu katika kuendesha shughuli zetu nchini Tanzania.” Mkurugenzi Mtendaji wa DPO Pay, Judy Waruiru alisema.

DPO Pay ambayo sasa ipo chini ya shirika la Network International, shirika ambalo ni wezeshaji mkuu wa biashara za kidigitali katika eneo la Afrika Mashariki na Kati iko tayari kutoa huduma zake nchini Tanzania.

Judy amebainisha utayari wa DPO Pay katika kuchagiza na kuwezesha ujumuishaji kifedha kwa makundi mbalimbali na ustawi wa biashara kidigitali.

Mifumo ya DPO ni thabiti na inahakikishia watumiaji wake kama wafanyabiashara kuweza kufanya miamala kwa urahisi, ufanisi, uhakika na haraka zaidi huku ikihakikishia watumiaji wake ulinzi wa taarifa zao.

“DPO Pay ina mifumo  thabiti inayohakikisha ulinzi wa taarifa za mtumiaji na ubora wa huduma. Kwa kutumia DPO Pay Mobile inayopatikana (istore/playstore), wateja wetu wanauhakika wakupata huduma mbalimbal katika ubora na upekee,” alisisitiza Judy.

DPO Pay tayari inafanyakazi Zanzibar na kutumiwa na wafanyabiashara wa hoteli, usafiri na watu binafsi kuupokea na kufanya malipo kupitia DPO Pay.

Huduma za DPO Pay zinatoa fursa kubwa kwa wafanyabiashara, na watu binafsi kuendesha malipo kidigitali ndani na nje ya nchi. Kwa sasa DPO Pay inaendesha shughuli zake katika nchi 20 barani Afrika. Pia kupitia DPO Pay, mteja anaweza kufanya malipo kupitia kadi ya benki, simu, kuhamisha fedha n.k.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Patricia J. Sawyers
Patricia J. Sawyers
2 months ago

Cash generating easy and fast method to work in part time and earn extra $15,000 or even more than this online. By working in my spare time I made $17,000 in my previous month and I am very happy now because of this job. You can try this now by follow.
.
.
Details Are Here——————————–>>> https://fastinccome.blogspot.com/

barketognu
barketognu
2 months ago

 my buddy’s mother-in-law gets $80 an hour on the internet. she has been without work for 12 months but last month her earnings was $16778 just working at home for a few hours per week.. check out this site—————– http://www.dailypro7.com

DorisSpadaro
DorisSpadaro
2 months ago

Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet… 

Check The Details HERE….. https://onlineweb76.blogspot.com/

LaraKerr
LaraKerr
2 months ago

I make 100 bucks per hours while I’m courageous to the most distant corners of the planet. Last week I worked on my PC in Rome, Monti Carlo at the long final in Paris. This week I’m back inside the USA. All I do fundamental errands from this one cool area see it. For more information,

Click on the link below………… https://Bestdollar4.blogspot.Bom

Last edited 2 months ago by LaraKerr
Back to top button
4
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x