MSHAMBULIAJI Roberto Firmino amejiunga na Al-Ahli ya Saudia Pro League kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea Liverpool.
Mbrazil huyo, 31, alikuwa huru baada ya mkataba wake na Liverpool kumalizika mwishoni mwa msimu ulioisha mwezi Mei.
Firmino amefunga mabao 111 katika michezo 362 akiwa na ‘The Reds’ tangu alipojiunga akitokea Hoffenheim ya Ujerumani mwaka 2015.
Anakua mongoni mwa wachezaji mwenye jina kubwa kujiunga na klabu hiyo baada ya Edouard Mendy kufanya hivyo.