KLABU ya Yanga imemtangaza Miguel Gamondi kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo akichukua nafasi ya Nasreddine Nabi.
Yanga imetangaza kocha huyo raia wa Argentina kwenye mkutano mkuu unaendelea muda huu.
Timu alizowahi kufundisha Gamondi ni Wydad, CR Belouizdad, Mamelodi Sundowns, CR Belouizdad, USM Alger, Espérance, Al-Ahly kama kocha msaidizina nyinginezo.