RAIS wa Liberia George Weah amekubali kushindwa katika uchaguzi na kiongozi wa upinzani Joseph Boakai baada ya ushindani mkali wa urais.
Boakai, makamu wa rais wa zamani ambaye alishindwa na Weah katika uchaguzi wa 2017, aliongoza kwa asilimia 50.9 ya kura dhidi ya Weah 49.1%, huku takriban kura zote zikiwa zimehesabiwa, tume ya uchaguzi nchini humo ilisema Ijumaa.
“Muda mfupi uliopita, nilizungumza na rais mteule Joseph Boakai kumpongeza kwa ushindi wake,” Weah alisema kwenye redio ya taifa. “Nawaomba muige mfano wangu na kukubali matokeo ya uchaguzi.
Comments are closed.