UTAFITI uliofanya na mtandao wa CIES Football Observatory, mfungaji bora wa Manchester City na Ligi Kuu ya England Erling Haaland, anaongoza orodha ya wachezaji ghali zaidi duniani..
Mshambuliaji wa Real Madrid, Vinicius Jr ameshika nafasi ya pili wakati mshambuliaji wa Arsenal Bukayo Saka akiwa kwenye nafasi ya tatu.
Kiungo wa Dortmund, Jude Bellingham anayehusishwa kujiunga na Real Madrid amewekwa nafasi ya nne.
Rodrigo Goes pamoja na viungo wa klabu ya Barcelona Pedri Gonzalez pamoja Pablo Gavi. Jamal Musiala, Phil Foden na Kylian Mbappe wakikamilisha orodha ya kumi bora.