Hospitali SUA inavyotegemewa upasuaji wanyama

Hospitali ya Taifa ya Rufaa ya Wanyama ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), iliyopo mkoani Morogoro imeendelea kutegemewa  nchini na  Watanzania  pamoja  na wageni wa nje ya nchi kuwezesha  uchunguzi wa magonjwa ya wanyama, matibabu na upasuaji wakiwemo  wanyamapori wanaovunjika baada ya kugongwa na magari .

Wabunge wa Kamati ya Kudumu  ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo  wamepata fursa ya kutembelea Hospitali hiyo ya Taifa ya Rufaa Machi 15, 2023 na kujionea mbwa anafanyiwa upasuaji  mdogo na madaktari bingwa wa wanyama wakiongozwa na  Dk Felix Martin  katika chumba cha upasuaji cha hospitali hiyo.

Advertisement