Hospitali Ushetu yaanza huduma upasuaji

HOSPITALI ya Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama mkoani Shinyanga,  kwa mara ya kwanza imeanza kutoa huduma ya upasuaji ya uzazi,  ambayo ilikuwa haipatikani  tangu kuanzishwa kwa halmashauri hiyo mwaka 2012.

Mganga mkuu wa halmashauri hiyo  Dk Athumani Matindo,  alisema wamefanya upasuaji kwa mama mmoja na kufanikiwa kumtoa mtoto salama.

Advertisement

Dk Matindo alisema mnamo mwezi Juni mwaka 2022, hospitali  ilianza kutoa huduma za kliniki ya  uzazi takribani wajawazito 150 wamejifungua kwa mwezi kwa njia ya kawaida sasa imeanza huduma ya upasuaji.

“Wajawazito walikuwa wakilazimika kusafiri kilomita 60 kufuata huduma ya upasuaji  hospitali ya Manispaa ya  Kahama, sasa huduma wataipata hapa bila wasiwasi wowote,”alisema Dk Matindo.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *