RAIS Samia suluhu Hassan amefungua Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mjini Magharibi (Lumumba), Zanzibar leo Januari 10, 2023.
Uzinduzi wa hospitali hiyo ni sehemu ya shamrashamra za kuelekea kwenye kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar.
Ujenzi wa hospitali hiyo ambayo itahudumia zaidi ya wananchi 800,000 imegharibu ya sh billioni 32.5 ambazo ni sehemu ya fedha za mkopo zilizopokelewa na Tanzania kwa ajili ya kukabiliana na athari za UVIKO19.