IAA watangaza udhamini wa masomo kozi 5 mpya

KATIKA kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan, Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kimetangaza udhamini wa masomo katika kozi mpya tano za kimkakati kwa mwaka 2023/2024

Akitangaza udhamini huo leo Agosti 24, 2023 jijini Dar es Salaam, Mkuu wa chuo hicho Profesa Eliamani Sedoyeka amesema kozi hizo ni shahada ya ukaguzi wa hesabu na uhakikisho, shahada ya media anuwai na mawasiliano kwa umma, shahada ya usimamizi wa nyaraka na taarifa, shahada ya usimamizi wa mikopo na shahada ya ukutubi na sayansi ya taarifa.

Profesa Sedoyeka amesema udhamini huo unawalenga wahitimu wa kidato cha sita kwa mwaka 2022 na 2023 wenye ndoto na malengo ya kusomea fani tajwa na wale wanaokabiliwa na changamoto za kifedha.

Aidha, ametaja vigezo vya kupata udhamini huo kuwa ni muombaji awe na ufaulu mzuri katika mtihani wa kidato cha nne na sita, usawa wa kijinsia, uthibitisho wa uhitaji wa msaada wa udhamini wa masomo.

“Vigezo hivyo pekee havitoshi ni lazima muombaji atoe maelezo ni kwa nini anadhani anastahili kupata mkopo, kusema hana uwezo haitoshi, atoe sababu za kutushawishi zaidi.” amesema Sedoyeka na kufafanua:

” Mfano kuna mwandishi mzuri wa michezo lakini ana Diploma hivyo angependa kusoma shahada ya Media Anuwai na Mawasiliano kwa Umma, anatueleza uzoefu wake katika uchambuzi wa michezo hivyo anaona akipata udhamini huo akaongeza elimu atakuwa bora, vigezo kama hivyo, ” amesema.

Profesa Sedoyeka amesema pia, ili muombaji akidhi vigezo vya kupata udhamini ni lazima awe ameomba kujiunga na chuo cha IAA na kufanya udahili.

“Dirisha la udahili awamu ya pili limefunguliwa rasmi leo Agosti 24 hadi Septemba 3, 2023.” amesema Prof. Sedoyeka

Prof. Sedoyeka ametoa wito kwa wanafunzi wote wenye Nia na hamasa ya kusoma katika chuo hicho cha IAA kuchangamkia fursa hiyo na kuomba udhamini.

…….

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Felicia
Felicia
1 month ago

Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet…

Check The Details HERE….. https://earncash82.blogspot.com/

Last edited 1 month ago by Felicia
FaithMysie
FaithMysie
1 month ago

 earn 200 dollars per hour working from home on an online job. 99 I never thought I could accomplish it, but my best friend makes $10,000 per month doing this profession and that I learn more about it.
CLICK HERE ——————-> http://www.SmartCash1.com

AnglinaKevin
AnglinaKevin
28 days ago

KAMATI YA LAAC YARIDHISHWA MRADI WA KITEGA UCHUMI cha WAGANGA WA KIENYEJI WA BIL. 67 JIJI LA DODOMA

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imeridhishwa na ujenzi wa Jengo la Kitega Uchumi CHINANGALI kwa shilingi bilioni 67 lililojengwa kwa lengo la kuongeza mapato ya ndani ya WAGANGA WA KIENYEJI TANZANIA.

MapinduziI.JPG
Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x