Ikongosi FC mshindi Negro Bonanza

TIMU ya soka ya Ikongosi (Ikongosi FC) imejinyakulia seti moja ya jezi na mpira wa kisasa baada ya kuibamiza kwa bao 1-0 Itulavanu FC katika fainali ya Negro Bonanza iliyopigwa katika uwanja wa kijiji cha Lugongo katika kata ya Ikongosi wilayani Mufindi.

Diwani wa kata ya Ikongosi, Negro Sanga aliyedhamini bonanza hilo lililohusisha pia mpira wa pete, mbio za kwenye magunia na kufukuza kuku ametumia bonanza hilo kutoa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Washindi wa michezo hiyo walijinyakulia fedha taslimu ya kati ya Sh 20,000 na Sh 100,000 huku wakiomba bonanza hilo liwe linafanyika kila baada ya miezi miwili.

Akikabidhi zawadi kwa washindi Sanga amesema anatambua michezo ni afya lakini pia ni ajira kama itaendelezwa ipasavyo.

“Mpira wa miguu ni njia nzuri ya kukuza vipaji vya wachezaji. Kuendeleza michezo kwa vijana hutoa fursa ya kujifunza stadi za timu, ushirikiano, na uongozi. Pia, inaweza kusaidia katika kujenga afya bora na kutoa jukwaa la kujifunza maadili kama nidhamu na kujitolea,” amesema.

Sanga ameishukuru serikali ya Dk Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha katika kata yake kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu, afya, maji, umeme, barabara na nyinginezo.

Akizungumzia hali ya maisha ya vijana wengi wakiwemo waliomaliza vyuo vikuu, alisema kilimo kinaweza kuwa chanzo kizuri cha ajira kwa vijana.

“Kupitia miradi ya kilimo, vijana wanaweza kujifunza na kushiriki katika uzalishaji wa chakula na mazao ya biashara, huku wakichangia pia kwenye maendeleo ya kilimo endelevu. Serikali na mashirika yanaweza kusaidia kutoa mafunzo na kutoa rasilimali ili kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika sekta hii ya kilimo,” alisema.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
EmmaJones
EmmaJones
18 days ago

Making extra salary every month from house more than $15,000 just by doing simple copy and paste like online job. I have received $18,000 from this easy home job. Everybody can now makes extra cash online easily.
.
.
By Just Follow———————————————————>>>  http://Www.BizWork1.Com

Angila
Angila
17 days ago

Making every month extra dollars by doing an easy job Online. Last month i have earned and received $18539 from this home based job just by giving this only mine 2 hrs a day. Easy to do work even a child can get this and start making money Online. Get this today by follow instructions
.
.
.
On This Website……………..> > http://remarkableincome09.blogspot.com

Scholarship ya Mwanadamu mwenye
Scholarship ya Mwanadamu mwenye
17 days ago

Scholarship ya Mwanadamu mwenye akili ya ‘Kinyonga mdogo zaidi duniani’ aliyegundulika Tanzania

Kinyonga kwa jina Brookesia urefu wake ni milimita 13.5

Wanasayansi wanaamini kuwa wamebaini kinyonga mdogo zaidi duniani ambaye ukubwa wake ni sawa na mbegu.

Vinyonga hao wawili ilibainika nchini Madagasca na timu ya sayanasi ya Ujerumani na Madagasca.

Kinyonga wa kiume aliyepewa jina la Brookesia urefu wake ni milimita 13.5.
Na kinyonga huyo anakuwa mdogo zaidi kati ya spishi karibu 11,500 za vinyonga, kulingana na rekodi ya hifadhi ya wanyama ya taifa ya Bavaria katika mjini mkuu wa Munich.

Urefu wake kutoka juu hadi chini ni milimita 22.
Kinyonga wa kike ni mkubwa kidogo takribani milimita 29, taasisi hiyo imesema, ikiongeza kwamba aina nyingine bado hazijapatikana, licha ya kwamba “juhudi zimekuwa zikiendelea”.

“Kinyonga huyo mpya aliyepatikana kaskazini mwa Madagascar eneo la msitu linalopokea mvua kubwa, huenda yuko katika hatari ya kutoweka,” kulingana na jarida la wanasayansi.

Oliver Hawlitschek, mwanasayansi wa kituo historia huko Hamburg, alisema: “Kwa bahati mbaya eneo alilokuwa akiishi mjusi huyo lilianza kuingiliwa na binadamu lakini likaanza kulindwa hivi karibuni, kwahiyo anawezaa kunusurika.”

Watafiti walibaini kwamba kinyonga huyo alikuwa anatafuta mchwa katika msitu wenye mvua kubwa na kujificha dhidi ya wanyama wala nyama usiku kwenye nyasi.
Katika msitu ambao mjusi Brookesia alipatikana umepakana na misitu mingine kaskazini mwa kisiwa, walisema.

Katika ripoti yao, wanasayansi wamependekeza kuwa kinyonga huyo aorodheshwe kama mnyama aliye hatarini katika orodha ya Shirika la IUCN, linalochunguza hali ya maelfu ya jamii za wanyama kumsaidia kumlinda na makazi yake.

Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x