Jaji Masaju, Dk Mayunga wateuliwa

RAIS Samia Suluhu Hassan amemteua Jaji George Masaju kuwa Mshauri wa Rais masuala ya sheria. Jaji Masaju ni Jaji wa Mahakama Kanda ya Dodoma
Taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Zuhura Yunus iliyotolewa leo Aprili 21, 2023 inasema kuwa uteuzi huo wa Jaji Masaju umeanza jana Aprili 20,2023.

Aidha, amemteua Dk Richard Mayungi kuwa mshauri wa Rais, masuala ya Mabadiliko ya Tabia nchini na Mazingira, kabla ya uteuzi huo Dk Mayungi alikuwa Meneja wa Mazingira, katika Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). uteuzi huo umeanza rasmi Aprili 19, 2023




