MAKAMU wa Rais wa Marekani Kamala Karris amewasili Dar es Salaam usiku wa Jumatano kwa ziara yake rasmi ya kiserikali ya siku tatu. Alikaribishwa na Makamu wa Rais wa Tanzania Dk. Phillip Mpango katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).
Ndege ya Air Force Two, toleo maalum la C-32 ya Boeing 757-200 iliwasili Tanzania kutoka Ghana ambako Bi Harris alitumia siku tatu za kwanza za ziara yake barani Afrika. Pia anatarajiwa kuzuru Zambia kabla ya kusafiri kwa ndege kurudi Marekani.