Kijiji cha Kiafrika kuanzishwa Urusi

URUSI, Moscow: Sehemu ya kijiji kati ya Moscow na St.
Petersburg imetengwa kuwa eneo la ‘Kijiji cha Kiafrika’ taarifa kutoka Urusi zimesema zikinukuu maadhimio ya kongamano la kimataifa la Afrika nchini humo – African International Congress.
Kijiji hicho ni sehemu ya mpango wa majaribio wa miaka mitano wa kusuluhisha maelfu ya wahamiaji kutoka Afrika Kusini.
Wanadiplomasia wa Kiafrika waliungana na wawakilishi wa AIC na maafisa wa serikali za mitaa kutoka Mkoa wa Tver wiki iliyopita kwa hafla ya kuzindua jiwe la msingi la kijiji hicho, ambalo litajengwa karibu na kitongoji cha Porechye.
“Tunapanga kuanzisha makazi 30 nchini Urusi kwa Waafrika wanaotaka kuhamia,” alisema mkuu wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Eurasian (EIU) na mwakilishi mkuu wa AIC nchini Urusi, Konstantin Klimenko.
“Hawa ni Boers, wakulima wenye asili ya Uropa, ambao mababu zao waliishi Afrika miaka mingi iliyopita,” Klimenko alielezea. “Wengi wao sasa wanageukia dini ya Othodoksi na kuhamia Urusi, wakivutiwa na njia yetu ya maisha na maadili ya kiroho, na kitamaduni ya familia.”
Afrovillage ni sehemu ya mradi wa majaribio unaoendelea hivi sasa katika mikoa ya Moscow na Tver, kwa lengo la kusuluhisha takriban familia 3,000 za Boer. Ikifanikiwa, AIC na washirika wake wanapanga kuipanua hadi mikoa mingine ya Urusi.