Kila baada ya dakika 8 mwanamke mmoja hufariki kwa kutoa mimba

KILA baada ya dakika nane, mwanamke mmoja hufariki dunia kutokana na utoaji mimba.

Hii ni licha ya viwango vya vifo vinavyosababishwa na matatizo ya uzazi kupungua kwa theluthi moja katika miaka 20 iliyopita.

Akizungumza katika Kongamano la wadau wa masuala ya Afya ya Uzazi lililoandaliwa na Chama cha Wanasheria Wanawake Tawla, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili(MUHAS), na bingwa wa magonjwa ya wanawake, Profesa Andrea Pembe amesema wanawake katika bara la Afrika ndio wanaongoza kufariki kwa hutoaji mimba usio salama.

Amesema, katika kila dakika moja kuna wamama wanne wanatoa mimba kwa njia ambazo sio salama.

“Na katika kila dakika 8 basi kuna mama ambaye anafariki kutokana na utoaji mimba. Wengine wanashindwa kupata ujauzito kwa sababu ya matatizo ambayo yametokana na utoaji mimba.”Anasema

Anasema wanawake milioni 56 utoa mimba duniani. Watatu kati ya wanne wapo bara la Afrika ambapo wanawake hao wapo hatarini zaidi kupoteza maisha  ukilinganisha na mabara mengine.

“Lakini si suala la kufa peke yake katika kila mama mmoja anakufa wengine upata matatizo ya muda mrefu kama ugumba.

“Duniani kwa ujumla unaweza kusema mwaka 2014 kulikwa na jumla ya utoaji mimba usio salama kwa wanawake million 42 na kati ya hizi nyingi zipo bara la Afrika.”

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) viwango hivyo  vilipungua pakubwa kati ya mwaka 2000 na 2015. Lakini vilisimama kwa kiasi kikubwa kati ya mwaka 2016 na 2020. Katika mataifa mengine hali ilidorora na kurudi nyuma.

Kwa jumla viwango vya vifo vya kina mama vilipungua kwa asilimia 34.3 katika kipindi cha miaka 20 kutoka vifo 339 kati ya wajawazito 100,000 mnamo mwaka 2,000 hadi vifo 223 katika mwaka 2020.

Licha ya sheria kukataza utoaji mimba, vitendo hivyo hufanyika na mara nyingi kwa njia zisizo salama

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Kim
Kim
2 months ago

I am now making $19k or more every month from home by doing very simple and easy job online from home. I have received exactly $20845 last month from this home job. Join now this job and start making cash online by

Follow instruction on website Here. . . . . . . .>>> http://www.Richcash1.com

Last edited 2 months ago by Kim
Dawn K. Walker
Dawn K. Walker
Reply to  Kim
2 months ago

I work an online job from home and earn 185 dollars per hour. I never imagined I could do it, but my best friend, who makes $15,000 a month at the job, encouraged me to find out more about it. This has limitless possibilities.
.
.
Details Are Here—————->>> https://Fastinccome.blogspot.com/

Julia
Julia
2 months ago

Earn income while simply working online. Work from home whenever you want. Just for maximum 5 hours a day you can make more than $600 per day online. From this I made $18,000 last month in my spare time.
.
.
Detail Here—————————————————————->>> http://Www.OnlineCash1.Com

Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x