Kila siku watu 200 huambukizwa VVU Nchini

DAR ES SALAAM: Kwa mujibu wa takwimu ya Ripoti ya viashiria vya maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) na UKIMWI ya mwaka 2016/2017 inaonesha kuwa kila siku nchini Tanzania, watu 200 huambukizwa VVU.
Kati yao asilimia 40 ni vijana wenye umri kati ya miaka 15-24, hata hivyo vijana wakike wanaongoza katika maambukizi hayo kwa asilimia 70-80.
Hayo yameelezwa na Mwezeshaji kutoka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Dk. Patrick Kanyamwenge kwa niaba ya Mratibu wa TACAIDS Mkoa wa Dar es Salaam, Hafidh Ameir katika semina wezeshi kuhusu elimu ya UKIMWI kwa watumishi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) iliyofanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tawi la DUCE, Temeke-Dar es Salaam.
Aidha, mwezeshaji huyo amesema malengo ya sasa ya nchi ni kuhakikisha ifikapo 2025 inafikia malengo ya dunia ya 95, 95, 95 (asilimia 95 ya watanzania wawe wamepima na kutambua hali zao, asilimia 95 ya waliogindulika na VVU wawe wameanza kutumia Dawa za kufubaza makali ya VVU, na asilimia 95 ya wanaotumia dawa wawe wamefubaza makali ya VVU)
Hata hivyo, Dk. Kanyamwenge amewaasa watumishi hao kuhakikisha wanajilinda na kuwalinda wengine na maambukizi dhidi ya VVU, pia kutoa elimu kwa watanzania.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
MelindCrabtree
MelindCrabtree
1 month ago

Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet… 

Check The Details HERE…..  https://earncash82.blogspot.com/

Last edited 1 month ago by MelindCrabtree
Vivian Wood
Vivian Wood
1 month ago

Our site covers a variety of topics, including digital marketing, business, technology, influencer marketing benefits and more. Our goal is to provide our readers with insightful and informative content that helps them stay up-to-date on the latest trends and developments in these fields.

SevynLennon
SevynLennon
1 month ago

They pay me $285 per hour to work on a laptop. e76 I had no clue it was possible, but a close friend made $26,000 in four weeks working on this simple offer, and she convinced me to try it. For further information, please see.
Details Are Here===========> http://www.SmartCash1.com

JulianaLopez
JulianaLopez
1 month ago

Earn more than $15,000 per month from home by simply copying and pasting an internet job. I was paid $18,000 for this basic work-from-home bs04 position. Everyone may now easily earn additional money online.
.
.
Detail Here———————————————————>>>  http://Www.OnlineCash1.Com

Back to top button
4
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x