Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Bunge leo jijini Dodoma imewasilisha ripoti yake baada kuwahoji viongozi wa Wizara ya Elimu na Teknolojia na Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB).
Akiwasilisha ripoti hiyo Bungeni, mjumbe wa Kamati hiyo kuwa, Mussa Ramadhani Sima hakuna ushahidi unaonesha hakukuwepo ushahidi unaoonesha kuwa Bodi hiyo ilikaidi maelekezo ya Waziri wa Elimu na Teknolojia, Prof Adolf Mkenda.
Spika Dk Tulia Ackson alilazimika kuiagiza Bodi hiyo Kamati hiyo kuwahoji viongozi wa Wizara hiyo pamoja na Menejimenti ya Bodi ya Mikopo kuona ikiwa HESLB imekaidi maelekezo kutoka wizarani au la.
Kwa mujibu wa Sima, kilichobainika ni kutowepo kwa mawasiliano mazuri baina ya pande zote mbili ambapo imeshauri jambo hilo lifanyiwe kazi.