Kinana amlilia Lowassa
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana, ametia saini kitabu cha maombolezo, katika msiba wa Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa.

Kinana amewasili nyumbani kwa Hayati Lowassa kijijini Ngarash leo Februari 16, 2023 na kutoa pole kwa familia, ndugu jamaa na wananchi wa Monduli.
Lowassa anatarajiwa kuzikwa kesho.




