Kituo cha Afya Maili Tano kujengewa kisima

Chatanda amesema hayo  baada ya kutembelea kituo hicho na  kufurahishwa na ujenzi wa wodi ya mama na mtoto katika kituo hicho.

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) Mary Chatanda amesema Kituo  cha Afya cha Maili tano katika wilaya Tabora Mjini kitajengewa kisima kuondokana na changamoto ya maji iliyopo kwa sasa.

Chatanda amesema hayo  leo baada ya kutembelea kituo hicho na  kufurahishwa na ujenzi wa wodi ya mama na mtoto katika kituo hicho.

” Nimefurahishwa na ujenzi huu lakini kuna changamoto ya maji katika kituo hiki, nimempigia Naibu Waziri Marryprisca Mahundi na kuniahidi  atachimba kisima hapa  hivi karibuni na itakuwa mwisho wa changamoto ya maji katika Kituo hiki, “amesema.

Advertisement

Ameeleza kuwa ameona aanze na  la maji  kwa kuwa wanawake wengi wanaojifungua katika kituo hicho  lazima watakuwa wanapata shida sana katika kupata maji safi na salama,  hivyo sasa wanawake na wananchi  Maili Tano changamoto ya maji itaisha.

2 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *