KOCHA Mkuu wa Simba SC, Abdelhak Benchikha amewasili Tanzania usiku huu tayari kuanza majukumu yake mapya.
Kocha huyo raia wa Algeria, amewasili akiwa na kocha msaidizi Farid Zemiti na kocha wa viungo Kamal Boudjenane.
Siku chache tatu zilizopita, Simba ilitangaza kupata kocha mpya akichukuwa nafasi ya Roberto Oliveira ‘Robertinho’ ambaye aliondoka klabuni hapo kwa makubaliano ya pande mbili.