Kumekucha Malinyi! hadi raha

MOROGORO: SERIKALI kuu imeipatia  Halmashauri ya Malinyi, iliyopo mkoani Morogoro gari jipya la kisasa la  kubeba wagonjwa (Ambulance) ukiwa ni  mpango makakati katika kuboresha  huduma za afya kwa wananchi.

Mbunge wa Jimbo la Malinyi , Antipas Mgungusi amesema kuwa, awali aliiomba  serikali kuu kupatiwa magari manne ya kubeba wagonjwa kwa ajili ya vituo vya afya Ngoheranga, Itete, Mtimbira, na Hospitali ya Wilaya ya Malinyi.

Mgungusi amesema, kutokana mambo ya bajeti amepatiwa gari moja kutoka  Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Advertisement

Mbunge huyo, amesema licha ya kupatiwa gari hilo , Wizara ya Afya nayo imeahidi kuwapatia Wananchi wa Malinyi gari jingine la kubebea wagonjwa ndani ya miezi miwili ijayo.

“Ninaimani kuwa gari hili  litatumika kwa matumizi sahihi yaliyokusudiwa na mheshimiwa Rais ya kusaidia Wananchi wa Wilaya ya Malinyi katika sekta ya Afya” amesema Mbunge Mgungusi .

Kwa upande wake  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi , Rehema  Bwasi , baada ya kukabidhiwa kwa gari hilo , ameishukuru  Serikali ya awamu ya sita wa kuwapatia gari hilo.

Amesema kuwa gari hilo litasaidia uboreshaji wa huduma za afya kwa  wagonjwa na matumizi ya Hospitali ya Wilaya, na kwamba  litatunzwa   na kutumika  kwa matumizi sahihi.

Bwasi ,amesema gari hilo litasaidia  kubeba wagonjwa kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya  na hivyo kuondoa changamoto iliyokuwepo awali kabla ya ujio wa gari hilo.

 

 

 

11 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *