Kutumia X Dola 1 kwa mwaka New Zealand, Ufilipino

MTANDAO wa X unaanzisha malipo ya kila mwaka ya US$1 kwa watumiaji wapya nchini New Zealand na Ufilipino kama sehemu ya mipango ya kuongeza mapato.

Imeelezwa hatua hiyo itasaidia “kupambana na roboti na watumaji taka kwenye X”, usajili, unaoitwa ‘Not A Bot’, unahitaji watumiaji wapya kuthibitisha utambulisho wao kwa nambari ya simu kabla ya kulipa ada ya kila mwaka au kuchagua akaunti ya malipo.

Taarifa ya mtandao wa Proactive wa Uingereza imeeleza kuwa ambao hawajajiandikisha kwa mpango huo wataweza kutumia programu ya mitandao ya kijamii kukamilisha kazi za ‘kusoma-tu’ kama vile kutazama machapisho na kutazama video.

Matokeo kutokana na jaribio yatashirikiwa hivi karibuni ingawa haijathibitishwa kwa nchi zingine, kufaulu kunaweza kusababisha kupitishwa ulimwenguni kote.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Back to top button
2
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x