LIVERPOOL itakuwa na kibarua kigumu kwa mara nyingine baada ya kupangwa na Real Madrid katika hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya droo iliyotolewa hivi punde.
Mchezo mwingine wenye hisia kali ni PSG ambaye amepangwa na Bayern Munchen.
Manchester City imepangwa na Leipzig, wakati Chelsea ikipangwa na Dortmund.
Tottenham Spurs imepagwa na AC Milan, wakati Inter Milan ikipangwa na FC Porto.
Frankfurt na Napoli, Club Brugge na Benfica.