Maaskofu wakemea mahubiri ya uongo

MAASKOFU wa Kanisa la Anglikan Tanzania wamekemea chimbuko la makanisa yanayoeneza mahubiri ya uongo na kujinufaisha kupitia ongezeko la watanzania wanaodanganyika kupata mali bila kufanya kazi na changamoto zao zingine kushughulikiwa kwa haraka.

Pamoja na mahubiri ya uongo, maaskofu hao wamezungumzia mmomonyoko wa maadili na anguko la mila na desturi za watanzania wakisema mambo hayo yakiachwa yaendelee taifa litaangamia.

Wameyasema hayo leo kwenye kongamano lao la kitaifa la uinjilisti linalofanyika katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa, mjini Iringa ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya kanisa hilo nchini.

Askofu wa Anglikan Dayosisi ya Ruaha (Iringa), Dk Joseph Mgomi alisema kanisa limewaita katika kongamano hilo wainjilisti hao kutoka nchi nzima ili wakae pamoja, kushauriana, kubadilishana uzoefu na maarifa yatakayowaweza kubadili mbinu itakayosaidia kufikisha injili ya kweli kwa wananchi.

“Injili ni ile ile iliyoandikwa karne ya kwanza na mpaka leo haijabadilika-lakini jamii tunayoihudumia inabadilika kila siku na sehemu yake imeanza kujitenga na imani ya kweli kwasababu kuna sauti nyingi zimeibuka zinazofundisha mahubiri ya uongo na kishetani,” alisema Askofu Dk Mgomi.

Alisema wanaofanya kazi hiyo ya kueneza mahubiri hayo wanafanikiwa kama alivyofanikiwa shetani kwasababu wanachanganya uongo na ukweli kidogo na hivyo kuziteka roho za watanzania wengi hususani wanawake.

Naye Askofu Julius Lugendo wa Kanisa Anglikana Dayosisi ya Southern Highlands (Mbeya), alisema kongamano hilo litasaidia kuleta umoja wa kanisa na uamsho kwa wainjilisti kufanya kazi ya kueneza injili ya kweli na kwa haraka ili kuinusuru jamii isiendelee kuhangamia.

“Tunaishi katika nyakati ngumu zilizojaa uharibufu wa kila namna na maadili yamepotea, hivyo ni muhimu tukawawezesha wainjilisti wetu wakaeneze injili katika nyakati hizi zilizobadilika ili tuwe na taifa lenye amani, staha na kumcha mungu kwa njia za kweli,” alisema.

Askofu Lugendo alisema dunia na Tanzania ya sasa imejaa mafundisho mengi yasio ya kweli na binadamu wanayakimbilia mafundisho hayo kwasababu yanawapa matumaini ya uongo yaliyojaa Imani ya kujipatia vitu au mali bila kufanya kazi na kuponya matatizo yao mengine.

“Kuna wahubiri wanaowaambia waumini wao wafungue pochi na baada ya muda fulani fedha zitajaa bila kufanya kazi yoyote. Uongo kama huu umeendelea kuaminiwa na wananchi wengi na tunaona jinsi Taifa linavyoelekea kuhangamia, hivyo ni lazima sisi kama kanisa tuchukue hatua,” alisema.

Alisema baada ya kongamano hilo, wainjilisti hao watashuka katika ngazi ya jamii na kuielimisha namna ya kujiondoa na mafundisho ya uongo, kufanya kazi na kumcha Mungu ili kuleta matokeo chanya kwa Taifa.

“Kwa kupitia kongamano hili tutajitahidi pia  kuelimisha watu wetu umuhimu wa kutunza mila na desturi zetu nzuri katika kupambana na uharibifu unaoosababisha ukatili wa kijinsia, kushamiri kwa vitendo vya usagaji na ushogan na baadhi ya watanzania kukataa kutambua jinsi zao hatua inayowafanya wanaume wanaishi kama wanawake na wanawake kama wanaume,” alisema.

Kwa upande wake Askofu Johnson Chinyong’ole wa Dayosisi ya Shinyanga alisema mpango wa kanisa hilo kueneza injili ya kweli kwa watanzania inatekelezwa kupitia mkakati wao unaolenga kuifikia kila kata ifikapo mwaka 2027.

“Katika maeneo mengi wapo watu wengi bado hawajamjua Mungu wa kweli na ndio maana wanahangukia katika mahubiri ya uongo. Kwa utafiti wetu tutahitaji kufika pia katika shule zote, vyuo vya kati na vyuo vikuu,” alisema.

Askofu Chinyong’ole alisema mpango huo wa kueneza injili kwa watu wote utawafikia pia wasomi wa fani mbalimbali nchini kote ambao ni waumini wa dhehebu hilo.

“Kutokana na kasi ya kuenea kwa mahubiri ya uongo tunatengeza watu watakaosimama na kuliombea Taifa ili lisiendelee kuhangamizwa na mahubiri ya uongo,” alisema.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Sarah
Sarah
2 months ago

finish some internet providers from home. I absolutely never thought it would try and be reachable anyway. My comrade mate got $13k just in about a month effectively doing this best task and furthermore she persuaded me to profit. Look at additional subtleties going to
this article..__________ http://Www.Careers12.com

Last edited 2 months ago by Sarah
Deanna Morgan
Deanna Morgan
2 months ago

I have a home-based business and make a respectable $60k per week, which is incredible given that a year ago I was unemployed due to a poor economy. I was given these instructions as a gift, and it is now my ne-02 responsibility to spread kindness and make them available to everyone.
This Page Provides Details—————>>> https://workscoin1.pages.dev/

MONEY
MONEY
2 months ago

MTONYO:- NHC, WATUMISH HOUSING, TBA TWENDE ZAMBIA

144.Mheshimiwa Spika, vilevile, Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2022/23 imeanza kutekeleza mradi wa kuendeleza viwanja vya Serikali jijini Lusaka, Zambia kwa kiasi cha Kwacha 500,000,000 (takriban shilingi bilioni 66.1) kwa kutumia utaratibu maalumu katika ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Zambia. Mradi huu unahusisha ujenzi wa majengo 10 kama inavyoonekana kwenye Kiambatisho Na. II cha Hotuba hii. Hadi Aprili 2023 Wizara imekamilisha tathmini ya zabuni za kampuni za ushauri elekezi zilizowasilisha maombi ya kuonesha nia (expression of interest) ya kusanifu majengo hayo. Zabuni ya kazi ya usanifu wa majengo hayo imetangazwa mwezi Mei 2023, na tuzo ya zabuni kwa kampuni zilizoshinda inatarajiwa kutolewa mwezi Juni 2023

Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x