Mabao 23 yameingia michezo Uefa

MABAO 23 yameingia kambani katika michezo minane ya raundi ya kwanza, siku ya kwanza michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Katika michezo hiyo, Barcelona amempa Royal mabao 5-0 katika dimba la Camp Nou.

Mchezo wa mapema AC Milan na Newcastle uliisha sare ya bila kufungana.

Manchester City ikiwa Etihad iliichapa Crvena mabao 3-1. PSG ikaichapa Dortmund mabao 2-0 uwanja wa Parc Des Princess.

Shaktar Donetsk ikiwa nyumbani ililala mabao 3-1 dhidi ya FC Porto. Feyernood akashinda mabao 2-0 dhidi ya Celtic.


Young Boys ikiwa nyumbani iliambulia kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa RB Leipzig, wakati Lazio wakiwa nyumbani wakaambulia sare ya mabao 1-1 dhidi ya Atletico Madrid.

Advertisement
4 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *