RAPA wa Bongo Fleva, Ahmadi Ali ‘Madee’ ametangaza kuacha kuimba muziki.
Mkongwe huyo aliyetamba na wimbo wa Pombe Yangu mwaka 2013, ametangaza uamuzi huo leo Juni 22, kupitia ukurasa wake wa Twitter.
Msanii huyo anayejiita Rais wa Manzese amesema ameamua kuachana na mambo yote na kwa kuanza ameamua kuacha kuimba.
“Umri wangu umekwenda sana na namshukuru Mungu kwa huu muda alionipa kwa sababu nimeshuhudia marafiki wengi sana hawakubahatika kufika 40” amesema Madee.
“Umaarufu mbaya sana nmeamua kuacha yote.”