Madereva wafundwa kuzingatia sheria

MADEREVA wametakiwa kutii sheria za usalama barabarani huku ikielezwa asilimia kubwa ya ajali zinatokana na harakati za kulipita gari jingine ‘overtake’.

Hayo yamesemwa Jana na Meneja wa Kitengo cha Usalama Barabarani kutoka makao makuu ambapo alisema alama za barabarani madereva wengi wamekuwa hawazitii kutokana na uzembe.

Daffa alisema mwendokasi kwa madereva pia unachangia ajali  michoro imechorwa ambayo inaonyesha uendelevu, kuna kona kali lakini dereva anang’ang’ania kutoka nje ya michoro huku akiwa mwendokasi unao hatarisha.

Advertisement

“Tanroads imefanya  juhudi  za kupunguza ajali kwa kuweka alama  za barabarani ambapo imekuwepo changamoto ya alama za kugongwa  au kuibiwa nondo zilizosimikwa barabarani.”alisema Daffa.

Mtaalamu kutoka kitengo  cha  mizani  makao makuu Tanroads, Vicent Tarimo amesema kufuatia sheria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya udhibiti uzito wa magari ya mwaka 2016 na kanuni zake za mwaka 2018  ambazo zimeanza kutumika hapa nchini mwezi Machi mwaka  2019.

“Uzito uliopitiliza katika gari  ni chanzo pia cha watu kupata  ajali hivyo wananchi  wanatakiwa wakiona hali hiyo watoe taarifa ili kuweza kuokoa maisha yao kwani yapo magari yanayobeba abiria yakiwa na mzigo uliopitiliza uzito”alisema  Tarimo.

Tarimo amesema magari  yenye uzito wa kuanzia 4.5 yanatakiwa yapite mizani  na Ile desturi ya gari kujaza abiria na kuwafaulisha  pembeni  kukwepa mizani watu hao wakibainika wachukuliwe Sheria.

2 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *