Mafuriko yaua 13 Ufilipino

VIFO vya watu vilivyotokana na mafuriko vimefikia 13 huku zaidi ya 45,000 wakiokolewa na kuhifadhiwa kwenye vituo maalumu, wengi waliopotea ikitaarifiwa ni wavuvi huko nchini Ufilipino.

Vifo hivyo vinajumujuisha mtoto wa mwaka mmoja na mzee wa miaka 64, eneo la kusini mwa Jimbo la Misamis. Mafuriko hayo yamesababishwa na mvua ya siku mbili yameathiri watu 166,000

Mkuu wa shirika la maafa katika mji wa Clarin jimbo la Misamis Occidental, alikiambia kituo cha redio cha DZBB kwamba shughuli za uokoaji zinaendelea na pamoja na kuokoa baadhi ya maeneo yaliyokuwa na shughuli za kilimo.

“Uharibifu mkubwa hapa ni mifugo,” Meya wa mji wa Clarin Emeterio Roa alisema kwenye redio.

Ofisi ya hali ya hewa ya nchi hiyo, Utawala wa Huduma za Anga ya Ufilipino, Jiofizikia na Unajimu (PAGASA), imesema  mvua kubwa inatarajiwa kunyesha katika maeneo ya nchi, na maporomoko ya ardhi yanayosababishwa na mvua kuna uwezekano katika baadhi ya maeneo yakaathirika zaidi.

Habari Zifananazo

3 Comments

  1. Do you have a spam issue on this site; I also am a blogger, and I was curious about your situation; we have developed some nice methods and we are looking to trade techniques with other folks, why not shoot me an e-mail if interested.

  2. Hi excellent blog! Does running a blog similar to this require a lot of work? I’ve virtually no expertise in computer programming however I was hoping to start my own blog soon. Anyhow, should you have any suggestions or techniques for new blog owners please share. I understand this is off topic however I simply needed to ask. Cheers!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button