Mahakama yaweka mikakati mipya kuepuka makosa ya kiufundi

MOROGORO: MAHAKAMA Kuu ya Tanzania imeweka jitihada kubwa katika kuhakikisha Majaji na Mahakimu nchini wanaondokana na makosa ya kiufundi yanayosababisha majangili kuachiwa hata pale wanapokutwa wamefanya makosa kwa kutoa adhabu isiyostahili.
Hayo yameelezwa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mustapher Siyani mjini Morogoro kupitia hotuba yake iliyosomwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro, Latifa Mansoor.
Jaji Mfawidhi Mansoor alimwakilisha Jaji Kiongozi kufungua mafunzo ya siku tano yaliyoanza ya uendeshaji mashauri ya makosa ya Wanyamapori na Maliasili yanayofadhiliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Pams Foundation kwa kushirikiana na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA).
Mafunzo hayo yanawashirikisha washiriki 157 ambao ni Majaji, Maofisa wa Mahakama, Waendesha mashitaka pamoja na Wapelelezi.
Alisema ,Mahakama imekuwa ikiwashughulikia majangili wakiwemo wa meno ya tembo na nyaraka za Serikali ambao hufikishwa mahakamani na kuhukumiwa, kifungo chake huwa ni miaka 20 na fidia kwa serikali.
Amesema kuna baadhi ya kesi ambazo hazijapelelezwa ipasavyo na kuwafanya majangili kutoka kwa ajili tu kuna makosa ya kiufundi katika upelelezi , hivyo mafunzo hayo yanalenga kuondokana na makosa ya kiufundi na kuhakikisha majangili wanapata adhabu inayostahili.
Hivyo amesema majangili wanapojitajirisha kupitia wanyamapori na misitu kiharamu wasiposhughulikiwa , faida wanazozipata zinatumika katika vitu vingi haramu ikiwemo kufanya ugaidi na kuwezesha vitu vingi haramu duniani.
Pamoja na hayo amesema, zipo juhudi zinafanywa na Shirika la Uhifadhi Tanzania (TANAPA) pamoja na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kuhifadhi aina za wanyamapori waliopo kwenye hatari ya kupotoweka ikiwemo Nyati.
Naye Mkurugenzi wa Mafunzo wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto , Dk Patricia Kisinda amesema ,tangu kuanzishwa kwa mafunzo hayo jumla ya maofisa wa mashitaka, mahakama na wadau wengine 250 wamepatiwa.
“ Tumeanza na Mikoa mitano ya Morogoro, Mtwara, Lindi, Dar es Salaam na Pwani na lengo letu ni kuwafikia walengwa 757 kwa mwaka huu (2023)” amesema Dk Kisinda.
I make $100h while I’m daring to the furthest corners of the planet. Last week I worked by my PC in Rome, Monti Carlo finally Paris… This week I’m back in the USA. All I do are basic tasks from this one cool site. see it,
Copy Here→→→→→ http://Www.Smartcash1.com
★They pay me $285 per hour to work on a laptop. ( s00q) I had no clue it was possible, but a close friend made $26,000 in four weeks working on this simple offer, and she convinced me to try it. For further information, please see.
Click and Copy Here══════►►► http://Www.SmartCareer1.com
I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com