Majaliwa akutana na wafanyabiashara Kariakoo

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amefika Kariakoo kuzungumza na Jumuiya ya wafanyabiashara wa soko hilo, badala ya Mei 17, 2023 kama ofisi yake ilivyotoa taarifa hapo awali.

Majaliwa amefika eneo hilo kuzungumza kuhusu mgomo wa wafanyabiashara hao pamoja na kero zinazowasumbua

Asubuhi ya leo wafanyabiashara hao waligoma kufungua maduka kwa madai ya utitiri wa kodi na tozo walizodai kutokuwa rafiki.

Taarifa ya awali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu ilieleza kuwa Majaliwa alipanga kukutana na uongozi wa jumuiya hiyo katika ukumbi wa Anatouglou uliopo Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *